Sunday, March 20, 2016

Kwa jumla kuna chaguzi 5 barani Afrika



Image copyrightReuters
Image captionMpiga kura
Uchaguzi unafanyika katika nchi tano za Afrika huku Senegal ikiandaa kura ya maoni kupunguza muhula wa rais.
Duru ya pili ya uchaguzi wa urais inafanyika nchini Niger, licha la mgombea upinzani kuwa hospitalini nchini Ufaransa.
Nchini Tanzania katika kisiwa cha Zanzibar, duru ya pili ya uchaguzi wa urais inafanyika baada ya kufutwa kutokana na matatizo yaliyotokea mwezi Oktoba
Uchaguzi pia unafanyika nchini Benin, Cape Verde na Congo Brazzaville.
Image copyrightGetty
Image captionUsalama umedumishwa kisiwani Zanzibar
Rais Muhamadou Issoufou anatarajiwa kushinda muhula wa pili katika kura ya kumpinga waziri mkuu wa zamani na spika wa bunge Hama Amadou.
Wakati wa duru ya kwanza mwezi Februari bwana Issoufou alipata asilimia 48 ya kura huku bwana Amadou akiwa wa pili na asilimia 17.
Usalama ni mkali kisiwani Zanzibar kutokana na kushuhudiwa ghasia wakati wa uchaguzi wa hivi majuzi.
Mwandishi wa BBC kisiwani humo anasema kuwa wapiga kura sio wengi vituoni . Chama cha upinzani cha CUF kimewashauri wafuasi wake kususia uchaguzi huo.
Matokeo ya mwezi Oktoba ya yalikataliwa baada ya mgombea wa CUF Seif Sharif Hamad kujitangaza mshindi kabla ya kutangazwa kwa matokeo rasmi.
Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment