Tuesday, March 29, 2016

EgyptAir yatekwa nyara: abiria atishia kulipua mkanda wake


Ndege ya shirika la ndege la Misri EgyptAir kwenye lami ya uwanja wa ndege wa Larnaca, Cyprus, Machi 29, 2016.
Ndege ya shirika la ndege la Misri EgyptAir kwenye lami ya uwanja wa ndege wa Larnaca, Cyprus, Machi 29, 2016.
REUTERS/Yiannis Kourtoglou


Ndege ya shirika la ndege la Misri EgyptAir iliyokuwa imebeba abiria 81 na wafanyakazi 7 ikifanya safari kati ya Alexandria na Cairo ambayo ilikua imetekwa nyara na watu wasiojulikana imetua katika mji wa Larnaca, nchini Cyprus.

Taarifa hii ni kwa mujibu wa runinga ya serikali ya Cypus na mamlaka ya uwanja wa ndege wa Cairo.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, abiria wa Misri
wanasadikiwa kuwa wameondolewa katika ndege hiyo mjini Larnaca.
Shirika la habari la Ufaransa la AFP limebaini kwamba abiria ametishia kulipua mkanda wake kwa mujibu wa vyanzo vya mamlaka ya usafiri wa anga.
Watekaji nyara waliwasiliana na maafisa mamalaka ya uwanja wa ndege saa 8:30 asubuhi saa za Cyprus (sawa na saa 5:30 asubuhi alfajiri saa za kimataifa) na ndege hiyo aina ya Boeing 737-800, ambayo ilikuwa ikifanya safari kati ya Alexandria na Cairo ilipewa kibali cha kutua saa 8:50 asubuhi, polisi imesema.

Watekaji nyara hawajazungumza chochote na kikosi cha askari polisi kimetumwa katika uwanja wa ndege wa Larnaca.
TAGS: MISRI - CYPRUS - ABDEL FATTAH AL-SISI
Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment