Tuesday, March 29, 2016

Israeli yasalimu amri kuhusu balozi wa Brazil



Image copyrightAFP
Image captionIsraeli yamuondoa balozi aliyekataliwa Brazil
Israel imelazimika kufutilia mbali uteuzi wa mlowezi wa kiyahudi kuwa balozi wake nchini Brazil baada ya taifa hilo kukataa kumpokea.
Brazil ilipinga na ikakataa katakata kumpokea balozi huyo mteule kutokana na msimamo wake mkali dhidi ya wapalestina.
Aidha Brazil ilisema kuwa Dani Dayan ambaye aliongoza unyakuzi wa mashamba ya wapalestina katika ukanda wa ukingo wa Magharibi unamnyima uwezo wa wastani kisiasa.
Waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu, amesma kuwa Dani sasa ataihudumia taifa hilo la kiyahudia katika ubalozi wake wa New York Marekani.
Image copyrightReuters
Image captionBrazil ilikatalia mbali uteuzi wake mwezi Agosti.
Brazil ilikatalia mbali uteuzi wake mwezi Agosti.
Kauli hiyo kali ya Brazil wachanganuzi wanasema kuwa ilielezea wazi msimamo wao dhidi ya unyakuzi wa ardhi ya wapalestina.
Awali Netanyahu alikuwa ameonya kuwa angechukua msimamo mkali dhidi ya Brazil iwapo ingeendelea kumkataa balozi huyo.
Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment