Showing posts with label UDAKU. Show all posts
Showing posts with label UDAKU. Show all posts

Saturday, January 21, 2017

Dokii afuata nyayo za Stereo, amchana Darassa kuwa anampenda na yupo tayari kuolewa

Msanii wa filamu, Dokii ameamua kufuata nyayo za Stereo kwa kuamua kumchana rapper Darassa kuwa anampenda.

Muigizaji amedai kwa sasa anamkubali sana Darassa kupitia kazi yake ya muziki, lakini yuko tayari kuolewa naye endapo Darassa mwenyewe atahitaji hilo.
“Nampenda sana Darassa, i love him, nampenda kwa sababu ya kazi yake, lakini sijawahi kumwambia, he is handsome….Darassa mi nampenda kazi yake but is very handsome, so what do you expect?… Mie sina mtu kwa sasa, so kama Darassa akitaka kunioa, niko tayari, am ready coz he is handsome” Dokii alikiambia kipindi cha FNL cha EATV.
Dokii alisema hayo ili kufafanua kuhusu picha ambayo ameonekana akiwa amepiga na Darassa, picha iliyozua mjadala kutokana na kuwa katika pozi lenye utata.
Pia alifafanua kuhusu mahusiano yake na msanii Rich Mavoko, ambapo alisema Rich ni ndugu yake hivyo hawawezi kuwa wapenzi.
Wiki chache zilizopita, rapper Stereo alimchana rapper Chemical kuwa anampenda na yupo tayari kwa lolote.

Mtoto wa Ray, Jaden afuata nyayo za Tiffah na Nillan wa Diamond



Tiffah ni mtoto maarufu zaidi kwenye mtandao wa Instagram Afrika akiwa na followers zaidi ya milioni moja. Mdogo wake, Nillan naye anafuata nyayo zake akiwa na followers zaidi ya 99k sasa. Akaunti zao husimamiwa na mama yao, Zari na hutumia Kimombo.
Na sasa mtoto mwingine wa mastaa wa Bongo, Jaden naye amejiunga kwenye kundi la watoto wa aina hiyo.

Jaden ni mtoto wa Ray Kigosi na Chuchu Hans aliyezaliwa wiki hii na tayari amefunguliwa akaunti kwenye mtandao huo. Yake inasimamiwa na mama yake na kama Tiffah na Nillan, amewafollow wazazi wake tu.

Katika kufurahia zawadi ya mtoto, Ray ameendelea kuweka wazi furaha yake kwa kuandika: Nikikuangalia Mwanangu Jaden Nakuwa Na Furaha Isiyo Kifani Na Kunipa Nguvu Ya Kupambana Na Maisha Ili Uishi Vizuri.. Mtoto ana Raha Yake Jamani asikwambie mtu Nyie Puyangeni Tu.

Thursday, January 19, 2017

Kajala Masanja akanusha binti yake kuharibikiwa kimaadili, ni baada ya video ya Ngono kusambaa mtandaoni

Katika mitandao mbalimbali ya kijamii ipo video iliyosambaa ambayo inamuhusu binti mdogo wa chini ya miaka 18 akifanya mapenzi na mtu mzima ndani ya Gari.

Awali ilisemekana kuwa katika video hiyo binti aliyeonekana ni Paula Paul ambaye ni mtoto wa staa wa filamu Kajala Masanja hali ambayo ilimfanya muigizaji huyo kukanusha uvumi huyo.

Muigizaji huyo kupitia instagram ameandika:
"Hey everyone….jamani mimi sina shida na mtu kama akinichukia au akinisema mimi kwa kitu chochote kile…kwasababu najua binadamu kuongea mmezoea..ila katika kuongea kwenu,kuingilia na kujudge my life naomba msimuingize mtoto wangu…
"Sijawahi kumuomba mtu anisaidie kulea hata siku moja…mimi nimeona kuna video insambaa mnasema ni mwanangu na mnajua kabisa sie paula huyo ila ilimradi tu mfurahishe roho zenu…nilinyamaza…ila sasa naona mnakoelekea ni pabaya..mnahisi yeye hana moyo? Au mnahisi haumii?.
"Mwanangu anasoma na sitaki mumchanganye na mambo yenu ya kipuuzi…vitu vibaya mnavyo muombea mwanangu viwarudie wenyewe…leave my daughter alone jamani…give us a break..fanyani tu mambo yenu yatakayofanya mpate faida katika maisha”,