Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts
Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts

Sunday, April 9, 2017

Uganda yamshikilia mwanaharakati kwa kumkosoa mke wa raisi Museven

media


Janet Museven Waziri wa Elimu wa Uganda na mke wa raisi Yoweri Museven
Uganda inamshikilia mwanaharakati na muhadhiri wa chuo kikuu cha Makerere kwa kumkosoa mke wa raisi wa Uganda kupitia mtandao wa kijamii.
Stella Nyanzi alimkosoa Bi Janet Museveni, ambaye ni waziri wa elimu kupitia ukurasa wake wa face book baada ya serikali kusema inaandaa mpango wa kugawa taulo za kike kwa wasichana wanafunzi ambao wapo katika mazingira magumu ya kupata vifaa hivyo.
Msemaji wa polisi Emilian Kayima amethibitisha kukamatwa kwa Stela Nyanzi ambaye atafikishwa mahakamani siku ya jumatatu jijini kampala kwa matumizi mabaya ya mtandao na kuvunja sheria ya mawasiliano ya mwaka 2011.
Kwa mujibu wa Kayima Bi Stella Nyanzi amekuwa akichapisha masuala yanayotazamwa kama vita kupitia mtandao wa kijamii ambayo hayana maslahi kwa taifa.

Muzbekistan mtuhumiwa mkuu wa shambulio liliouwa wanne Sweden.

Mwanaume wa miaka 39 raia wa Uzbekistan mbaroni kwa tuhuma za kuiteka nyara lori na kulibamiza kwa umati mkubwa wa watu Stockholm na kuuwa watu wanne kujeruhi wengine 15 katika shambulio la kigaidi.
Mwanaume mwenye umri wa miaka 39 raia wa Uzbekistan alioko kizuizini ni dereva anayetuhumiwa kuliteka nyara la kusambaza bia ambalo liliuvamia umati mkubwa wa watu katikati ya mji mkuu wa Stockholm na kuuwa watu wanne na kujeruhi wengine 15 katika kile kinachoonekana dhahir kuwa ni shambulio la kigaidi.
Mwanaume huyo ambaye alikuwa akijulikana kabla na mashirika ya ujasusi ya Sweden ambaye ni mtu aliyejitenga asiekuwa na uhusiano unaofahamika na makundi ya Kislamu ya itikadi kali anatuhumiwa kuwaponda wapita njia katika mtaa wenye harakati kubwa za manunuzi na kulibamiza gari hilo hadi ndani ya duka moja hapo Ijumaa (07.04.2017).
Dan Elliason mkuu wa jeshi la polisi nchini Sweden ameuambia mkutano wa wandishi wa habari hapo Jummamosi kwamba hakuna kinachoashiria kwamba mtu huyo waliemkamata sie aliehusika na shambulio hilo na kwamba kinyume chake tuhuma zimezidi kuimarika wakati uchunguzi ukiendelea.
Mtu huyo aliekamatwa Ijumaa usiku kwa madai ya kuhusika na ugaidi baada ya kutokea shambulio katikati ya mji mkuu wa Stockhlom inaonekana alichukuwa hatua hiyo peke yake lakini mkuu huyo wa polisi amesema "bado hawafuti uwezekano watu wengine zaidi wakawa wanahusika."
Hakuwa na uhusiano na makundi ya kigaidi
Schweden - Stockholm nach dem Anschlag - Prinzessin Victoria (picture alliance/Lehtikuva/dpa/A. Aimo-Koivisto) Mwana mrithi wa ufalme Victoria nchini Sweden akiwasili na mwana mfalme Daniel katika eneo la maombolezo karibu na shambulio lilipotokea
Kwa mujibu wa shirika la habari la taifa TT mtuhumiwa huyo kutoka Jamhuri ya Uzbekistan ilioko Asia ya kati atawakilishwa na wakili atakayeteuliwa na mahakama Johan Eriksson.Polisi hauikutaja jina la mtuhumiwa huyo na kwamba inaonekansa alikuwa pembezoni mwa repoti za ujasusi.Mkuu wa polisi wa usalama wa Sapo Anders Thornberg amesema wamepokea taarifa za ujasusi mwaka jana lakini hawakuona uhusiano wowote na makundi ya itikadi kali.
Mkuu wa jeshi la polisi Eliasson amesema shambulio hilo linafanana kabisa na lile lililokea London mwezi uliopita ambapo kwayo watu sita wameuwawa akiwemo mshambuliaji mwenyewe ambaye aliendesha gari lililokuwa limekodiwa na kuwagonga wapita njia waliokuwepo katika daraja nje ya bunge la Uingereza.
Magari pia yametumiwa kama silaha katika mji wa Nice nchini Ufaransa na Berlin nchini Ujerumani mwaka uliopita katika mashambulizi yanayodaiwa kufanywa na kundi linalojiita kundi la Dola la Kiislamu.
Hakukuwa na taarifa iliyotolewa mara moja kudai kuhusika na shambulio hilo nchini Sweden ambayo hadi hisi sasa ilikuwa hauikuguswa na mashambulio makubwa ya kigaidi na ambapo wengi walikuwa wakijivunia kuwa ni taifa la kidemokrasia lililo na uwazi.
Kifaa chafanana na bomu la kienyeji
Schweden - Stockholm nach dem Anschlag - Dan Eliasson (Getty Images/AFP/TT/A. Wiklund) Mkuu wa jeshi la polisi Sweden Dan Eliasson -akizungumza na waandishi wa habari.
Polisi imesema imegunduwa kifaa chenye kutia shaka ndani ya gari hilo ambalo liliishia kujibamiza katika duka la Ahlens lakini imesema hawajui iwapo kifaa hicho lilikuwa bomu la kienyeji kama ilivyoripotiwa na kituo cha matangazo cha SVT.
Maafisa wa serikali za mitaa katika mji wa Stockholm ambapo bendera zimekuwa zikipepea nusu mlingoti kwenye majengo ikiwa ni pamoja na bunge na kasri la kifalme wamesema watu 10 akiwemo mtoto mmoja bado wanaendelea kupatiwa matibabu hospitali huku watu wazima wawili wakiwa kituo cha wagonjwa mahtuti.
Sweden hapo Jumatatu mchana itabaki kimya kwa dakika moja kuomboleza wale waliopoteza maisha yao.

Monday, April 3, 2017

Upinzani DRC waitisha mgomo wa kitaifa

Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo anatazamiwa kukutana na ujumbe wa upinzani kusaka njia za kuukwamua mkwamo wa kisiasa unaotishia kuyavunja makubaliano ya Disemba 31.
Hata hivyo, hakuna uhakika endapo upinzani utashiriki kwenye mazungumzo hayo yaliyoitishwa wakati upinzani nao ukipanga mgomo wa nchi nzima kumshinikiza Kabila kutekeleza kwa vitendo makubaliano hayo yaliyosimamiwa na Kanisa Katoliki nchini Kongo.
Wakati huo huo, mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, ametoa wito wa kupatikana kwa amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, akitaka umwagaji damu ukomeshwe mkoani Kasai.
"Taarifa za mapigano zinaendelea kuwasili kutoka Kasai, ambayo yanapelekea wahanga wengi zaidi na kuwakosesha watu makaazi yao," mkuu huyo wa Kanisa aliwaambia waumini wapatao 2,000 katika mji wa Carpi ulio kaskazini mwa Italia, ambao wenyewe ulikumbwa na matetemeko mawili makubwa ya ardhi mwaka 2012.
"Kila mmoja aombe ipatikane amani na kwamba nyoyo za wanaohusika na uhalifu huu zisibakie watumwa wa chuki na ghasia," alisema.
Watu wapatao 400 wamekufa ndani ya kipindi cha miezi sita ya machafuko ambayo yamesambaa kwenze majimbo ya Kasai-Central, Kasai, Kasai-West na Lomami.
Vatikanstadt - Papst Franziskus empfängt EU Vertreter (Reuters/Pool/A. Medichini) Papa Francis ataka kusitishwa kwa mauaji ya Kasanga, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Mkoa huu unakabiliwa na mapigano tangu vikosi vya serikali kumuuwa kiongozi wa kimila na mkuu wa kundi moja la wanamgambo, Kamwina Nsapu, katikati ya mwezi Agosti 2016. Nsapu anaripotiwa kuanzisha uasi dhidi ya serikali kuu ya Rais Joseph Kabila mjini Kinshasa.
Siku ya Alhamis (30 Machi), viongozi wa kanisa na mwakilishi wa Papa Francis nchini Kongo walivitaka vyombo vya usalama, ambavyo vinatuhumiwa kwa kuwatesa wapinzani, kujizuia kutumia nguvu kupita kiasi wakati wa operesheni zao.
Mwezi uliopita, polisi iliwatuhumu waasi kwa kuwauwa maafisa 39 jimboni Kasai, na wiki iliyopita miilki ya wahandisi wawili wa Umoja wa Mataifa ilipatikana baada ya kutekwa nyara huko Kasai-Central.
Raia wawili wa kigeni walitekwa na watu wasiojuilikana tarehe 12 Machi sambamba na raia wengine wanne wa Kikongo waliokuwa wanawasindikiza.
Bensouda asema uhalifu wa kivita umetendeka DRC
Fatou Bensouda Pressekonferenz (picture-alliance/dpa) Mwendesha Mashitaka Mkuu wa ICC, Fatou Bensouda, anaamini kuna uhalifu dhidi ya ubinaadamu unatendeka nchini DRC.
Katika hatua nyengine, mwendesha mashitaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), Fatou Bensouda, amesema kuuawa kinyama kwa timu ya wataalamu ya Umoja wa Mataifa na ghasia nyengine nchini Kongo kunaweza kuwa sawa na uhalifu unaoweza kushitakiwa na mahakama yake.
Katika taarifa yake ya Ijumaa, Bensouda alisema amesikitishwa sana ghasia kwenye jimbo la Kasai. Miili ya raia wa Marekani, Michael Sharp, Msweden Zaida Catalan, na mkalimani raia wa Kongo, Betu Tshintela, ilipatikana mapema wiki hii.
Wataalamu hao walikuwa wakichunguza tuhuma za uvunjaji wa haki za binaadamu uliofanywa na jeshi la Kongo na makundi ya wanamgambo kwenye eneo hilo.
Watu wengine watatu kwenye timu yao, bado hawajuilikani walipo, lakini Bensouda ameitaka serikali ya Kinshasa kufanya uchunguzi wa kina na "wa hakika".
Kawaida, ICC inaweza kutoa waraka wa kukamatwa kwa washukiwa, lakini ni juu ya taifa mwanachama kuwakamata na kuwafikisha mahakamani kujibu mashitaka.

Sunday, April 2, 2017

Umoja wa Mataifa warefusha jukumu la kulinda amani Kongo

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mabli na kurefusha jukumu la kulinda amani nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo pia linaazimia kupunguza idadi ya wanajeshi wake wa kulinda amani nchini humo.
Kura iliyopigwa jana inaazimia kupunguza idadi ya wanajeshi hao hadi kufikia 16,200.  Hatua hiyo imefikiwa ijapokuwa imepingwa na mahakama ya kimataifa ya uhalifu - ICC ambayo inachunguza uhalifu wa kivita katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo tangu mwaka 2014. Kwa mujibu wa mwendesha mashtaka mkuu wa ICC Fatou Bensouda mgogoro wa hivi karibuni pamoja na kuuwawa kwa wataalamu wawili wa kigeni wa Umoja wa Mataifa, ni wazi kuwa uhalifu wa kivita umetendeka.
Hadi watu 400 wameuwawa kutokana na kuendelea kwa mapigano yaliyoanza mwezi Agosti mwaka uliopita wakati majeshi ya serikali yalipomuuwa kiongozi mmoja wa kikabila aliyekuwa anampinga rais Joseph Kabila.
Niederlande Den Haag Gerichtsvollzieherin Fatou Bensouda beim Fall Jean-Pierre Bemba (picture-alliance/AP Photo/J. Lampen) Mwendesha mashtaka mkuu wa ICC Fatou Bensouda
 Bibi Bensouda ameelezea wasiwasi wake kutokana na ripoti mbalimbali juu ya machafuko mabaya yaliyotokea katika miezi kadhaa iliyopita nchini Kongo na hasa katika jimbo la Kasai. Bensouda ameyasema hayo katika taarifa yake aliyoitoa mjini The Hague. Mwendesha mashtaka huyo mkuu amesema hatasita kuchukua hatua za kisheria na ameapa kuawaadhibu wote wanaohusika.  Jimbo la kati la Kasai, ambako kiongozi wa kikabila Kamwina Nsapu aliuwawa mwaka uliopita, ndio kitovu hasa cha vurugu ambazo zimezagaa hadi katika mikoa mingine jirani ya Kasai-Oriental na Lomami.
Utekaji nyara na mauaji
Miili ya watalaamu wawili wa Umoja wa Matafia ilipatikana wiki hii.  Wataalamu hao walikuwa Mmarekani Michael Sharp na Zaida Catalan raia wa Sweden.  Watu hao waliripotiwa kupotea tangu mwanzoni mwa mwezi wa Machi. Mwili mmoja moja kati ya hiyo miwili ulikuwa umeharibika vibaya. Hadi kufikia sasa raia wanne wa Kongo waliokuwa wameandamana na  wataalamu hao bado hawajulikani waliko.  Mabalozi katika Umoja wa Mataifa walisema  wataalamu hao walikuwa wanachunguza taarifa juu ya makaburi ya halaiki.  Wiki iliyopita askari wapatao 39 pia walivamiwa na kuuwawa na waasi katika jimbo hilo la Kasai.
Bensouda amezitolea mwito pande zote kujiepusha na vitendo vya uhalifu wa kivita huku akiitaka serikali ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuwafungulia mashtaka waliohusika na mauaji hayo katika taifa hilo la Afrika ya Kati linalokabiliwa na machafuko.
Mahakama ya kimataifa ya uhalifu ya ICC ilianzishwa mnamo mwaka 2002 kwa ajili ya kuchunguza na hatimaye kuwafungulia mashitaka watu wanaofanya uhalifu mbaya duniani. Uchunguzi wao katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo umewezesha kuwafikisha watuhumiwa katika mahakamna hiyo ya kimataifa ya ICC na tayari hukumu zimeshatolewa katika kesi mbili.
Mbabe wa kivita Thomas Lubanga  alihukumiwa kifungo cha miaka 14 kutokana na kuwatumikisha watoto katika jeshi lake la waasi na Germain Katanga alifungwa miaka 12 kwa kuhusika na mapigano ya kikabila ya mwaka  2003 katika kijiji kimoja kwenye mkoa wa Ituri uliopo kaskazini mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.  Kesi ya mtuhumiwa wa tatu Bosco Ntaganda bado inaendelea. Ntagamba anakabiliwa na tuhuma18 za uhalifu wa kivita pamoja nakuwatesa binadamu. Mtuhumiwa huyo amekanusha tuhuma hizo dhidi yake lakini waendesha mashtaka wanasema alihusika na alikuwa kiungo cha kati katika machafuko ya Ituri.  Watu wapatao 60,000 wameuwawa tokea mwaka 1999, kwa mujibu wa taarifa za makundi ya kutetea haki.
Umoja wa Mataifa unamshinikiza rais Joseph Kabila kuheshimu makubaliano ya kugawana madaraka na upinzani kablaya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika baadae mwaka huu. Lakini mpaka sasa haijulikani iwapo rais Kabila ataachia madaraka mwaka huu. Umoja wa mataifa, Umoja wa Ulaya na Umoja wa Afrika wamehimiza kutajwa kiongozi mpya wa upinzani kulingana na makaubaliano yaliyofikiwa mwezi desemba mwaka uliopita.

Gigaba kutetea sera za chama cha ANC

Waziri mpya wa fedha wa Afrika Kusini Malusi Gigaba ameahidi kutekeleza sera za chama tawala cha ANC wakati chama hicho kikindelea kugawika vibaya kufuatia kutimuliwa kwa ghafla kwa waziri aliyemtangulia Pravin Gordhan.
Gigaba alichukuwa nafasi ya Pravin Gordhan aliyeondolewa katika wadhifa huo katika mabadiliko ya baraza la mawaziri ya ghafla usiku wa manane yaliyofanywa na Rais Jacob Zuma ambayo yameonyesha kuwepo mgawanyiko ndani ya chama hicho cha ANC.          
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Pretoria hapo Jumamosi (01.04.2017) Gigaba amesema "nitalenga sana  katika kutekeleza sera za ANC katika kuboresha maisha ya Waafrika kusini walio wengi."
Hapo mwaka 2014 chama hicho cha ANC kilipitisha ya sera za mageuzi makubwa ya kiuchumi katika juhudi za kuharakisha kushirikishwa katika shughuli kuu za kiuchumi wananchi wa Kiafrika walio wengi ambao huko nyuma walikuwa wametengwa.
Amesema kumezidi kuwepo na maafikiano ndani ya chama hicho tawala kwamba kasi na ukubwa wa mageuzi hayo imekuwa ya taratibu  mno na mara nyingi imekuwa haiendani na uhalisia.
Hana tajiriba ya kiuchumi
Südafrika | Präsident Jacob Zuma (REUTERS/S. Hisham) Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini.
Hata hivyo kuchaguliwa kwa Gigaba kumezusha wasi wasi miongoni mwa vyama vya upinzani na waanangalizi wa masuala ya kiuchumi kutokana na kwamba hana misingi ya masuala ya fedha na kwa kiasi kikubwa anaonekana kama ni mshirika wa Rais Zuma.
Gigaba pia amesema kwamba anajuwa kwamba kuna tazizo la kutokuwepo na imani na serikali kwa hiyo ameahidi kuwatowatelekeza wananchi kwa kuruhusu maslahi ya watu maalum kudhuru wananchi.Amesema dhima yake ni "kurudisha utulivu" . Waziri huyo wa zamani wa mambo ya ndani na mkuu wa jumuiya ya vijana ya ANC hana tajiriba kubwa ya kiuchumi lakini amekubali kukutana na Gordhan.
Sarafu ya randi ya nchi hiyo mojawapo ya mataifa yenye nguvu kubwa za kiuchumi barani Afrika imeshuka thamani kutokana na wasi wasi wa kuwepo kwa rushwa katika ngazi ya juu serikalini.
Waziri huyo mpya amesema amejitolea kushikilia nchi hiyo kuwa katika kiwango inachostahiki kupewa mikopo ya uwekezaji na kwamba amekuwa akizungumza na mashirika yenye kupima uwezo wa nchi kulipa mikopo yake.
Amesema anafahamu fika juu ya mazingira yalioko sasa ya kugawika kwa nchi hiyo na kuchochewa kisiasa na ameahidi kutoyumbishwa na masuala ya nje.
Pigo kuondolewa kwa Gordhan
Südafrika Sandton Finanzminister Pravin Gordhan (Reuters/S. Sibeko) Aliyekuwa waziri wa fedha Pravin Gordhan.
Kutimuliwa kwa Gordhan na naibu wake Mocebisi Jonas kumeelezewa na wakosoaji kuwa ni hatua iliyochukuliwa na Zuma kuwaweka wafuasi wake katika hazina.
Gordhan ambaye alikuwa akitetea utawala safi na alikuwa akiheshimiwa kimataifa kutimuliwa kwake kumezusha miito ya kumtaka Zuma ajiuzulu.Kuondolewa kwake wizara ya fedha ambako alikuwa ngome dhidi ya watu wanaotaka kuchota fedha hazina kwa maslahi binafsi ni pigo jengine kwa uchumi wa Afrika Kusini ambao ulikuwa tu kwa asilimia 0.5 mwaka jana ina ina kiwango cha ukosefu wa ajira cha asilimia 27.
Kuondolewa kwa mawaziri 10 katika mabadiliko ya baraza la mawaziri lenye mawaziri 35 kumezidisha fadhaa nchini Afrika Kusini ambapo fahari yake iko katika sifa zake za kidemokrasia zilizoundwa wakati wa mapambano dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi na ambazo zimefifia kwa miaka sasa kutokana na kashfa zinazomzunguka Zuma.
Makamo wa rais Cyril Ramaphosa amekosowa kutimuliwa kwa Gordhan katika kauli ya nadra hadharani kumlaumu rais.

Mahakama kuu ya Venezuela yabatilisha uamuzi wake wa awali

 Mahakama kuu nchini Venezuela imeghairi uamuzi wake juu ya kutwaa mamlaka ya bunge linalodhibitiwa na upinzani.  Uamuzi huo ulisababisha shutuma kutoka duniani kote. Maandamano makubwa yalifanyika nchini Venezuela.
Mahakama hiyo kuu ilisema katika uamuzi uliochapishwa kwenye tovuti yake kwamba imeibatilisha hukumu iliyoitoa tarehe 29 mwezi Machi juu ya kulinyng'anya bunge mamlaka, baada ya hukumu hiyo kusababisha wasiwasi kwamba Venezuela inaelekea kwenye udikteta chini ya rais wa mrengo wa shoto Nicolas Maduro.  Mahakama hiyo pia imeghairi uamuzi wake wa kuwaondolea wabunge kinga ya kisheria.
Hatua hiyo mpya imechukuliwa na mahakama kuu baada ya rais Nicolas Maduro kuitaka taasisi hiyo iupitie upya uamuzi wake na pia baada ya kufanyika mkutano juu ya usalama wa nchi hapo jana. Wapinzani na mkuu wa shirika la nchi za Amerika waliufananisha uamuzi wa mahakama kuu na kutwaa mamlaka kwa nguvu.  Uamuzi wa mahakama hiyo inayoegemea upande wa rais Maduro ulishutumiwa pia na Marekani, Umoja wa Ulaya, Brazil, Mexico , Argentina, Chile na Colombia.
Venezuelas Präsident Nicolas Maduro (picture-alliance/dpa/A. Rivera/P. Miraflores) Rais wa Venezuela Nicolas Madura
Uamuzi wa mahakama kuu wa jana ulionyesha mgeuko usio wa kawaida kwa rais Madura, Msoshalisti ambaye alionekana kuvuka mipaka katika njama zake za kutaka kuyaimarisha mamlaka yake.  Hata mwanasheria mkuu wa Venezuela Luisa Ortega, ambaye ni mshirika wa Maduro alipinga hatua ya kulinyag'anya bunge mamlaka. Ortega alieleza kuwa hatua hiyo ilikiuka taratibu za katiba.
Viongozi wa upinzani wamesema uamuzi wa mahakama kuu wa kughairi hukumu yake ni ushuhuda kwamba mfumo wa sheria unadhibitiwa na rais Maduro.  Kiongozi wa bunge Julio Borges amesema huwezi kujifanya unarejesha hali ya kawaida nchini baada ya kufanya mapinduzi.  Hapo awali bwana Borges aliichana hati ya uamuzi wa mahakama kuu kwenye mkutano na waandishi wa habari.
Katika uamuzi wake wa siku ya Jumatano mahakama kuu ya Venezuela ilisema wabunge waliidharau mahakama kwa kukataa kuyazingatia maamuzi ya hapo awali yaliyobatilisha sheria iliyopitishwa na bunge.
Mahakama hiyo kuu ya nchini Venezuela imetengua maamuzi kadhaa ya bunge na kulivua mamlaka  tangu wapinzani washinde uchaguzi uliofanyika mwaka 2015. Juhudi za mara kwa mara za wapinzani za kutaka kufanyika kura ya maoni na uchaguzi mpya kabla ya kumalizika kwa muhula wa rais Maduro zimekuwa zinapingwa na mahakama hiyo kuu pamoja na tume ya uchaguzi.  Muhula wa rais Maduro unamalizika mwaka 2019.
Kwa muda wa zaidi ya mwaka mmoja rais huyo amekuwa anaongoza kwa amri za dharura ili kukabiliana na mgogoro wa kiuchumi ambao umesababisha wasiwasi kwamba huenda Venezuela ikasambaratika na hivyo kusababisha hali mbaya ya kiusalama na maafa kwa binadamu katika kanda ya Amerika.

Aliyegundua vyombo vya muziki vya Roland, Ikutaro Kakehashi amefariki akiwa na umri wa miaka 87


 
Ikutaro Kakehashi aliunda mashine TR-808
Image caption Ikutaro Kakehashi aliunda mashine TR-808
Ulimwengu wa muziki unaomboleza kifo cha mwanzilishi wa vyombo vya muziki vya Roland Ikutaro Kakehashi, ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 87.
Mhandisi huyo raia wa Japan aligundua vyombo vingi vya kupiga ngoma kikiwemo chombo cha TR-808
Vyombo hivyo vimetumiwa kwa muziki wa hip-hop na kutumiwa na wanamuziki wrngi wakiwemo Kanye West hadi Marvin Gaye.
Kakehashi alipewa tuzo la kiufundi la Garmmy mwaka 2013 kwa mchango wake katika teknolojia ya muziki.
Kabla ya kuongoza Roland kwa miaka 40, bwana Kakehashi alianzisha kampuni ya Ace Tone miaka ya sitini..
Sauti ya chombo cha muziki cha TR-808 ilileta mabadiliko makubwa kwenye muziki miaka themanini na tisini.
Albamu yake Kanye West ya mwaka 2008 ya 808s & Heartbreak, inakionyesha chombo hicho wakati wote.
Haki miliki ya picha Facebook / Tommy Snyder
 
Ikutaro Kakehashi (picha ya juu, kushoto)
Image caption Ikutaro Kakehashi (picha ya juu, kushoto)

Watu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi Colombia


 
Watu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi Colombia
Image caption Watu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi Colombia
Mamlaka ya jeshi la Colombia inasema idadi ya waliofariki katika maporomoko ya ardhi nchini humo imefikia watu 250 huku waliojeruhiwa wakiwa 400.
Hata hivyo idadi hiyo huenda ikaongezeka kwani bado kuna zaidi ya watu 200 ambao hawajapatikana .
Vikosi vya wafanyikazi wanaoendesha shughuli za uokoaji wanasema nyingi ya barabara za kulipotekea maporomoko hayo huko eneo la mji wa kusini mwa taifa hilo, Mocoa hazipitiki kutokana na mkasa huo.
Watu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi Colombia
Image caption Watu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi Colombia
Maporomo hayo yametokea baada ya mvua kali kunyesha kwa saa nyingi.
Viongozi wa mataifa jirani wa Mexico na Argentina walikuwa wa kwanza kutoa ujumbe wa pole na kuahidi kwenda kuisaidia Colombia.
Rais Juan Manuel Santosa alitangaza hali ya tahadhari eneo hilo na kusafiri kuangalia shughuli za uokoaji.
Watu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi Colombia
Image caption Watu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi Colombia
Picha zilizochapisww kwenye mitandao na jeshi zilionyesha baadhi ya majeruhi wakiokolewa kwa kutumia ndege.
Maporomo koya ardhi yamekumba eneo hilo mara kadha miezi ya hivi karibuni.
Mwezi Novemba, watu 9 waliuawa kwenye mji wa El Tambo, karibu kilomita 140 kutoka Mocoa kufuatia maporomoko ya ardhi yaliyosababiswa na mvua kubwa.
 
Watu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi Colombia
Image caption Watu 250 waangamia kwenye maporomoko ya ardhi Colombia

UN yaongeza muda wa MONUSCO DRC

media
Wajumbe wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa wakipiga kura.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha kwa kauli moja azimio linaloongeza muda wa ujumbe wa umoja huo MONUSCO nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na kupunguza idadi ya askari wake.
MONUSCO imeongezewa muda hadi tarehe 31 mwezi Machi mwakani.
Kwa mujibu wa umoja wa mataifa azimio hilo limegusia suala muhimu lililokuwa linajadiliwa kuhusu kupunguza idadi ya askari, ambapo sasa imepunguzwa hadi askari 16,215.
Azimio limemtaka Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres kufanya tathmini ya majukumu ya MONUSCO kwa wakati huu kuona iwapo majukumu yote ni muhimu.
Wanachama wa baraza hilo wamemuonya raisi Joseph Kabila kwamba utawala wake lazima iheshimu mkataba wa kusirikiana uongozi na upande wa upinzani na kuruhusu uchaguzi muhimu kufanyika.
Balozi wa uingereza katika baraza la usalama la umoja wa mataifa Matthew Rycroft, ambaye alikuwa mwenyekiti wa baraza mwezi huu ameeleza kuwa ukosefu wa usalama na mvutano umeendelea kushuhudiwa katika kipindi chote nchini DRC.RFI

Tuesday, March 28, 2017

Malawi Yaichokonoa Tena Tanzania Kuhusu Ziwa Nyasa

Rais wa Malawi, Peter Mutharika ameanza tena chokochoko baada ya kutangaza kuwa hakuna nchi ambayo inamiliki kwa pamoja Ziwa Nyasa na kwamba haijafikia makubaliano na nchi yoyote, hivyo ameahidi kulinda umiliki na masilahi yake.

Kauli hiyo ni tofauti na mazungumzo ya Mutharika na Rais John Magufuli yaliyofanyika Januari 30 jijini Addis Ababa, Ethiopia wakati walipokuwa wakihudhuria kikao cha Umoja wa Afrika (AU).

Katika taarifa iliyotolewa na Idara ya Mawasiliano ya Rais baada ya kikao hicho, ilisema marais wote wameridhishwa na jitihada zinazofanywa na jopo la usuluhishi lililoteuliwa na Umoja wa Maendeleo wa Nchi za Kusini mwa Afrika (Sadc).

Jopo hilo linaongozwa na rais wa zamani wa Msumbiji, Joachim Chisano.

Mkuu wa kitengo cha mawasiliano katika wizara ya  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mindi Kasiga amekiri kuiona taarifa hiyo na alisema anayeweza kulizungumzia suala hilo ni Naibu Waziri.

“Tumeiona hiyo taarifa ila jaribu kumtafuta Naibu Waziri maana Waziri atakuwa nje ya nchi. Ninachofahamu baraza la usuluhishi bado linaendelea na vikao vyake. Ukimpata naibu waziri atakuwa na maelezo ya kina.”alisema Mindi.

Lakini, akihudhuria Siku ya Maji Duniani Jumatano iliyopita mjini Mangoshi, Rais Mutharika alisisitiza msimamo wa Malawi kulinda umiliki wa ziwa hilo dhidi ya watu aliowaita wavamizi.

Mutharika alisema Malawi ndiye mmiliki pekee wa Ziwa Malawi, ambalo huku linajulikana kama Ziwa Nyasa, na kuonya kuwa utawala wake hautavumilia watu watakaokuwa na nia ya kuyumbisha taarifa za umiliki.

“Hebu tulilinde ziwa letu. Hili ni ziwa letu na ninaposema ziwa letu namaanisha ziwa lote. Mtu yeyote asifanye kosa la kubadili umiliki ambao umekuwepo kwa miaka 124 iliyopita,” alisema Mutharika akikaririwa na tovuti ya Nyasa Times ya Malawi juzi wakati wa mkutano huo uliofanyika ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Nkopola Lakeshore mjini Mangochi.

“Tunathamini ziwa letu na tutahakikisha tunachukua hatua za kulilinda kwa gharama zozote,” alisema.

Mutharika aliwataka wananchi kupunguza matumizi mabaya ya maji ili yapatikane kwa ajili ya kilimo na viwandani wakati wa msimu wa ukame.

Hivi karibuni, Malawi na Tanzania zimejikuta katika mzozo wa umiliki wa Ziwa Nyasa lililo kusini mwa Tanzania, mzozo ambao umesababisha kuanza kwa mazungumzo ya usuluhishi kumaliza kutokubaliana huko baada ya nchi hizo mbili kushindwa kufikia muafaka. Mzozo wa mpaka kwenye Ziwa Nyasa umekuwepo tangu mwaka 1967.

Lakini, mzozo wa hivi karibuni umeibuka baada ya Malawi kuanza utafiti wa mafuta na gesi kwenye ziwa hilo.

Hata hivyo, Mutharika alisema uchimbaji mafuta utaendelea katika ziwa hilo licha ya wanaharakati wa mazingira kuitaka Malawi iache mpango huo.

“Wale wanaohofia kuhusu mipango yetu ya kutafuta na kuchimba mafuta hawana sababu ya kuhofia. Kama tutaamua kuchimba mafuta katika ziwa, tutahakikisha tunatumia teknolojia safi,” alisema akikaririwa na Nyasa Times.

Wednesday, March 22, 2017

Madaktari Kenya Wawaonya Madaktari wa Tanzania Wanaotaka Kwenda Kenya

Chama cha Madaktari wa Kenya (KMPDU), kimewataka wenzao wa Tanzania wasikubali kusaini mkataba wowote wa kwenda Kenya kabla mgogoro wao na Serikali haujatatuliwa.

Taarifa ya KMPDU  inasema haina tatizo na uwezo ama mafunzo ya madaktari wa Tanzania na protokali ya leseni za madaktari inayotambulika na Baraza na Bodi za nchi za Afrika Mashariki.

“Lakini tunapenda kuwataarifu kwamba kwa miaka miwili iliyopita, madaktari wa Kenya wamekuwa wakihangaika na Serikali ya Kenya kuhusu idadi yetu na kukataliwa kwa kile Serikali na Wizara ya Afya ilichosema ni ukomo wa bajeti jambo ambalo lilikuwa likichochea mgomo uliokwisha wiki moja iliyopita.

“Tunawashukuru kwa kutuunga mkono wakati wa mgomo wetu uliodumu kwa siku 100.

“Tumeona makubaliano ya Serikali ya Kenya na Tanzania wa kuleta madaktari 500 ili kuleta uwiano (ration) kati ya wagonjwa na madaktari kwenye pengo lililopo nchini kwa sasa.

“Hadi kufikia Mei 2017, kutakuwa na madaktari wanaokadiriwa kufikia 1,400 ambao hawajaajiriwa na Serikali ya Kenya,” ilisema taarifa hiyo.

Wakati huo huo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, alisema madaktari 159 nchini wametuma maombi ya kazi kwenda kufanya kazi nchini Kenya hadi sasa, tangu Serikali ilipotoa tangazo Machi 18, mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Ummy aliwatoa hofu madaktari kuhusu usalama wao wawapo nchini Kenya kutekeleza majukumu yao.

 “Rais Uhuru Kenyata ambaye ni mwenyeji wetu, amemuhakikishia Rais Dk. John Magufuli, kwamba tutakuwa salama,” alisema.

Ili kukamilisha suala hilo, alisema tayari wizara yake imeandaa rasimu ya makubaliano ambayo itaeleza mambo yote kimaandishi, likiwamo suala la usalama na masilahi yao waliyoahidiwa.

Alisema madaktari hao watakapoajiriwa nchini humo watalipwa mshahara sawa na madaktari wengine wa huko.

Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohamed Bakari, alisema kabla ya uamuzi huo kutolewa na kukubaliwa na nchi zote mbili, ulijadiliwa kwa kina faida na athari zitakazojitokeza.

“Kenya ilituhakikishia usalama wa madaktari wetu, mshahara mzuri pamoja na makazi ya uhakika, hivyo Serikali ilijiridhisha ni fursa nzuri ya ajira kwa madaktari wetu,” alisema Profesa Mohamed.

Msimamo wa MAT
Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), kimepinga uamuzi wa Serikali kuipatia madaktari 500 Kenya hadi hapo nchi hiyo itakapoanza kutekeleza makubaliano kati yake na madaktari wake ambao hivi karibuni waligoma kwa takribani miezi mitatu.

Taarifa ya MAT iliyotolewa juzi na Mwenyekiti wake, Dk. Obadia Nyogole, ilisema: “Kumekuwepo na maoni tofauti juu ya madaktari wa Tanzania kwenda Kenya, na zaidi ya asilimia 60 ya madaktari wa nchi hiyo wamepinga suala hilo na kutaka wazawa kwanza ndiyo waajiriwe."

Saturday, January 21, 2017

Trump alenga Obamacare

Rais wa Marekani Donald Trump ametia saini amri za serikali mojawapo ikiwa ni agizo linalolenga kuifuta bima ya Afya iliyoanzishwa na mtangulizi wake Barrack Obama maarufu kama Obamacare. Agizo hilo lenye lengo la kuipunguzia serikali mzigo wa kiuchumi, linaziamuru taasisi za kiserikali kukomesha hatua zitakazoendeleza bima hiyo inayofadhiliwa na serikali. Badala yake linataka taasisi hizo kupunguza, kuchelewesha au kufutilia mbali gharama za matibabu ambazo zilishughulikiwa na bima hiyo. Hatua ambayo itaweka gharama hiyo kwa serikali za majimbo na watu binafsi. Bima hiyo huwawezesha mamilioni ya wamarekani wasiojiweza kupata huduma ya afya kwa gharama nafuu. Kuiondoa kabisa bima hiyo kutahitaji mswada kupitishwa katika bunge la Marekani

Trump aanza kufanyia mabadiliko sheria za Obama


Trump na mkewe wakitembea Washington
image caption Trump na mkewe wakitembea Washington
Rais wa Marekani Donald Trump ameanza kutia saini maagizo ya rais, baadhi yake yakiwa ni ya kubadili yale yalioafikiwa na mtangulizi wake Barak Obama.
Muda mfupi baada ya kukagua gwaride la kuapishwa kwake, Bw Trump, alitia amri ya serikali, kupunguza mzigo wa kiuchumi kwa taifa, unaotokana na gharama za kufadhili bima ya matibabu ya bei nafuu inayofahamika kama Obamacare, ambayo Trump aliahidi kufanyia marekebisho.
Trump pia ametia saini amri ya kuwaidhinisha mawaziri wake wapya wa Ulinzi na usalama wa kitaifa ambao uteuzi wao umepitishwa na bunge la seneti.
Utawala wa Trump pia umeaanza kufanyia marekebisho mtandao wa kijamii wa Ikulu ya White House kwa kuweka masuala yatakayopatiwa kipaumbele na uongozi huo mpya.

VIDEO: Gari lilivyochomwa moto Washington DC. na waandamanaji wanaompinga Donald Trump

Wanasema haijawahi kutokea fujo za namna hii kwenye historia ya Marais wapya Marekani, hii imetokea kwenye mji wa Washington DC. wakati huu ambao Rais Donald Trump ameapishwa kuwa Rais wa 45 wa Marekani.
Waandamanaji wanaompinga waliandamana kwa wingi kwenye mitaa mbalimbali ya mji huo wakiwa na Mabango na wakipaza sauti kuonyesha wazi kwamba hawamtaki na wengine walivunja vioo vya Maduka, Magari na hata kuchoma moto gari moja la kifahari.
Katika kuonyesha kwamba hawaogopi, Waandamanaji hao walivunja mpaka kioo cha gari la Polisi lililopita katikati yao kama inavyoonekana kwenye hii video hapa chini, inasemekana hadi sasa ni zaidi ya Waandamanaji 100 wamekamatwa na Polisi.

Rais Wa Gambia Akubali Kuachia Madaraka

Yahya Jammeh ambaye amekua madarakani na kuingoza Gambia kama Rais kwa miaka 22 hatimae amekubali kuachia madaraka hayo na sasa Adama Barrow aliyetangazwa mshindi kwenye uchaguzi mkuu ndio anatarajiwa kuchukua nafasi.

Kupitia Television ya taifa, Yahya ametangaza kuachia madaraka ambapo AlJAZEERA wameripoti kwamba taarifa kutoka IKULU zilisema baada ya kuachia madaraka alitarajiwa kuondoka kwenye nchi hiyo ndani ya siku 3 ila media nyingine zinasema amepewa saa tu za kuondoka.

TV ya habari Nigeria imesema ECOWAS walimpa hadi saa sita mchana kuondoka lakini mwenyewe akaomba muda huo usogezwe hadi saa kumi jioni na imeripotiwa atakwenda kuishi Guinea.

Barrow aliandika kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Twitter na kusema ‘Yahya Jammeh amekubali kuachia madaraka na anatarajiwa kuondoka kwenye nchi ya Gambia leo’

Tuesday, September 13, 2016

Makamu Wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan Awasili Lusaka Kumwakilisha Rais Dkt. Magufuli Kwenye Sherehe Za Kula Kiapo Rais Wa Zambia Edgar Lungu


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akilakiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Vijana, Michezo na Maendeleo ya Watoto Mhe. Agnes Musunga mara baada ya kutua  katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kenneth Kaunda jijini Lusaka, Zambia, leo Jumatatu Septemba 12, 2016  tayari kwa kumuwakilisha Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt John Pombe Joseph Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa rais wa sita wa nchi hiyo Mhe. Edgar Lungu leo Jumanne Septemba 13, 2016 katika uwanja wa Mashujaa jijini Lusaka

Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea shada la maua  mara baada ya kutua  katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kenneth Kaunda jijini Lusaka, Zambia, leo Jumatatu Septemba 12, 2016  tayari kwa kumuwakilisha Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt John Pombe Joseph Magufuli kwenye sherehe za kuapishwa rais wa sita wa nchi hiyo Mhe. Edgar Lungu leo  Jumanne Septemba 13, 2016 katika uwanja wa Mashujaa jijini Lusaka.

Sunday, July 10, 2016

Simu milioni 10 za Android zaathiriwa na kirusi


Kirusi kinachoathiri simu za Android
Hadi simu milioni 10 aina ya Android zimeambukizwa virusi vinavyotoa Clicks bandia kwa ajili ya matangazo kulingana na watafiti.
Programu hiyo pia inaweka apps na kumchunguza mwenye akaunti.
Kirusi hicho kinawapatia takriban dola 300,000 kila mwezi waliokianzisha.
Simu nyingi ambazo zimeathiriwa na kirusi hicho zipo nchini China
Ongezeko la simu zilizoathiriwa na kirusi hicho lilibainika na kampuni ya usalama wa mitandao Checkpoint na Lookout.
Kirusi hicho kinatoka familia ya Shedun by Lookout but Hummingbad by Checkpoint.
Image caption Smartphone
Katika blogu,Checkpoint imesema kuwa imefanikiwa kubaini kithibiti cha simu zilizoathiriwa ambacho kinaonyesha kuwa Hummingbad imeathiri simu milioni 10.
China ,India,Ufilipino na Indonesia zinaongoza katika mataifa yenye simu zilizoathirika.

Boko Haram yashambulia kambi ya jeshi Nigeria


 
Image caption Jaribio la Boko Haram kushambulia kambi ya kijeshi Nigeria lilitibuka 16 kati yao waliuawa
Jeshi nchini Nigeria linasema kuwa limewaua wanachama 16 wa kundi la Boko Haram katika mapigano yaliyodumu saa kadhaa.
Msemaji wa jeshi alisema kuwa mapigano hayo yalianza wakati washambuliaji wa kujitolea mhanga waliokuwa wakitumia pikipiki walijaribu kuingia katika kambi ya jeshi eneo la Rann karibu na mpaka na Cameroon.
Image copyright BOKO HARAM VIDEO
Image caption Wapiganaji wa Boko haram walishambulia kambi ya kijeshi wakiwa na pikipiki na mabomu
Wanajeshi wawili waliuawa huku wenyeji wakisema kuwa raia 7 nao walipoteza maisha yao.
Harakati za Boko Haram ambazo zimedumu kipindi cha miaka 7 zimesababisha vifo vya takriban watu 20,000 kaskazini mashariki mwa Nigeria na kuwalazimu karibu watu milioni 2 kuhama makwao.

Mapigano yazuka upya Sudan Kusini


 
Image caption Hali bado ni tete Sudan Kusini
Msemaji wa jeshi tiifu kwa makamu wa rais wa Sudan Kusini Riek Machar ameiambia BBC kuwa majeshi yao yanakabiliana na jeshi la serikali tiifu kwa rais wa Sudan Kusini Salva Kiir.
Kanali William Gatjiath amesema kuwa wanajeshi watiifu kwa bw Machar wamevamia mji mkuu wa Juba kutoka pande zote .
Kanali Gatjiath anasema wanajeshi hao wanalipiza kisasi kufuatia mashambulizi makali kutoka kwa jeshi la rais Kiir.
Serikali haijasema lolote tangu machafuko hayo yaanze muda mchache uliopita.
Awali Wanajeshi wanamuunga mkono makamu wa rais wa Sudan Kusini Riek Machar walisema kuwa kambi yao ilishambuliwa usiku wa kuamkia leo kwa risasi na bunduki nzito nzito.
Image copyright Reuters
Image caption Rais Salva Kiir na makamu wa rais Riek Machar wamewasihi wafuasi wao kulinda amani
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini unasema kuwa kulitokea ufyatulianaji wa risasi katika mji mkuu wa nchi hiyo Juba..
Maeneo yanayodhaniwa kuathirika sana ni yale ya Jebal.
Ujumbe huo unasema kuwa ufyatulianaji mkubwa wa rasasi ulishuhudiwa karibu na kambi ya umoja wa mataifa
Siku za hivi majuzi ziaidi ya watu 100 wanaripotiwa kuuawa mjini Juba wakati wa mapigano kati ya wafuasi wa rais Salva Kiir na makamu wa rais Riek Machar
Wawili hao walikubaliana kumaliza vita vya wenywe kwa wenyewe na wametoa wito wa kuwepo utulivu.
Ripoti za awali kutoka nchini Sudan Kusini zilisema kuwa takriban watu 100 waliuawa wakati wa mapigano kati ya wanajeshi hasimu katika mji mkuu Juba.
Hata hivyo idadi kamili bado haijulikani lakini wengi wa wale waliouawa wanaripotiwa kuwa wanajeshi.
Mapigano hayo yaliyoanza siku ya Alhamisi yaliendelea hadi mapema Jumamosi.
Mwandishi wa habari mjini Juba anasema kuwa wanajeshi wameweka vizuizi vya barabarani mjini humo.
Anasema kuwa masoko yamefunguliwa lakini watu wengi wamebaki nyumbani.
Sudan Kusini inaadhimisha miaka mitano ya uhuru wake.

Sunday, June 26, 2016

Waethiopia 19 wapoteza maisha ndani ya lori la wasafirishaji haramu wa watu:IOM

Wakimbizi wa kutoka Ethiopia na Eritrea amabo wanaokolewa na wafanya kazi wa IOM.(Picha:© IOM 2015)
Takribani Waethiopia 19 wamekutwa wamekufa ndani ya lori nchini Zambia baada ya kukosa hewa . Lori hilo linasadikiwa kuwa ni la mtandao wa usafirishaji haramu wa binadamu na lilikuwa likielekea Afrika ya Kusini.
Kwa mujibu wa shirika la kimataifa la uhamiaji IOM , wahanga hao walikutwa baada ya manusura kugongagonga kontena walimokuwa wakihitaji msaada. Msemaji wa IOM Joel Millman amesema tukio hilo ni baya sana kulishuhudia.
(SAUTI YA JOEL MILLMAN)
"Hili ni kubwakabisa tunalolifahamu, lakini kumekuwa na visa vingine vya kutisha kwatika safari hizo siku za nyuma.Nadhani ilikuwa mwaka jana au miwili iliyopita kulikuwa na tukio la wahamiaji kuzama, ambao walishuhudiwa wakiliwa na mamba, lakini hatujawahi kuona vifo vya kukosa hewa kwenye kontena kama hivi"
Kwa mujibu wa IOM manusura 76 waliojumuisha watoto, wamepelekwa kwenye makazi ya dharura.