Tuesday, March 29, 2016
Sanaa ya vichekesho(Comedy) inaendelea kukua siku hadi siku lakini ukuaji wake una mambo mengi yanayo takiwa yabadilishwe,sio sisi watazamaji bali wao wenyewe wahusika waya badilishe ili waendane na soko la Dunia na kufikia ngazi za Mr Bean au Charlie Chaplin.
1.Nguo- hapo zamani sanaa hii ilikuwa huwezi kuchekesha hadi ujipake majivu au uvae makumburu(nguo zisizo na sura nzuri) huku lengo lao kubwa lilikuwa kuchekesha, japo walikuwa wanatembea na sahani kwa ajili ya zile shilingi kumi hamsini au mia watunzwe kama umependa alicho chekesha. dhana hii inatakiwa iishe japo imepunguzwa kwasababu kwa sasa sio wengi wanao chekesha kwa mfumo ule wa zamani.
2.Ubunifu- hapa ndio haswa changamoto kubwa ipo mtu hafikirii dunia inaendaje na inataka nini, kichekesho kinaweza kuwa hata kumtungia kiongozi wa nchi (Rais) ,mazingira au hata vivutio mbalimbali kwa njia ya kichekesho na ukapata pesa.
Mifano mizuri ipo Kitale ni mmoja wa watu wanaoweza kukidhi kiwango cha soko la kisasa haswa kwa ubunifu na uvaaji wake miongoni mwa wachekeshaji wote waangalie mfano mzuri wa Kitale pia wangalie Joti na Mpoki walifanya hatua zote za uchekeshaji walivaa nguo mbaya na sasa wana vaa nguo nzuri kwa lengo la kuendana na soko.
kila siku tuna hubiri umoja, upendo na ushirikiano pia wasiwe wabishi kuwafuata ambao wamefanikiwa mfano Kitale, jopo zima la Orijino komedi, Idriss Sultan na wengine walio acha kufanya kama zamani na kufanya kimataifa zaidi.
Unknown
Web Developer
Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment