Friday, March 18, 2016

Wapiganaji wa al-Shabaab wazingirwa Somalia



MapiganoImage copyrightAFP
Image captionMapigano makali yamekuwa takiendelea tangu Jumatatu
Wapiganaji takriban 200 waliokuwa wameshambulia eneo moja katika jimbo la Puntland, wamezingira na wanajeshi wa jimbo hilo.
Naibu rais wa jimbo hilo Abdihakim Amry ameambia BBC kwamba wanajeshi hao wamewapa wapiganaji hao agizo la kuwataka kujisalimisha la sivyo wakabiliwe.
Mapigano makali yamekuwa yakiendelea katika eneo hilo la Suuj, ambalo linapatikana katika mkoa wa Nugaal katika pwani ya jimbo hilo lililo na uhuru kiasi kutoka kwa Somalia.
Wapiganaji wa al-Shabaab walifika eneo hilo kwa boti na kuchukua udhibiti.
Wanajeshi watano wa Puntland wanaripotiwa kuuawa kwenye mapigano na wanamgambo hao katika eneo hilo.
Jana, kituo cha redio cha kibinafsi cha Radio Mustaqbal kilimnukuu Naibu Waziri Mkuu wa Somalia Mohamed Omar Arte akisema serikali kuu iko tayari kutuma wanajeshi wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika (Amisom) “kukabiliana na wapiganaji hao wa al-Shabab eneo la Puntland iwapo watahitajika”.
Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment