Tuesday, March 22, 2016

Taifa Stars ya Tanzania kuikabili Chad



Image captionTaifa Stars ya Tanzania kuchuana na Chad Jumatano
Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars itashuka dimbani hapo kesho, huko nchi Chad katika mchezo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2017.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa majira ya saa 11 kwa saa za nyumbani Afrika Mashariki.
Taifa Stars, imefanya mazoezi ya mwisho kuelekea mchezo huo katika uwanja wa Omnisports Idriss Mahamat Ouya ulipo katika jiji la D'jamena.
Kocha anayekinoa kikosi hicho Charles Boniface Mkwasa amesema anashukuru vijana wake hakuna majeruhi na wote wameweza kufanya mazoezi aliyoyapangilia.
Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment