Saturday, March 19, 2016

Mitt Romney:Cruz ndiye atakayemzuia Trump



Image copyrightAP
Image captionMitt Romney
Aliyekuwa mgombea wa urais nchini Marekani Mitt Romney amesema kuwa atampigia kura seneta wa Texas Ted Cruz kwa kuwa ''havutiwi'' na mgombea wa chama hicho aliye kifua mbele Donald Trump.
Bwana Romney amesema katika mtandao wake wa facebook kwamba njia ya kipekee ya kumchagua mgombea wa Republican ni kupitia mkutano ambapo wanachama wanamchagua atakayegombea kupitia chama hicho.
Image copyrightEPA
Image captionDonald Trump na Mitt Romney
Alifanya kampeni na Gavana John Kasich huko Ohio lakini akasema kuwa kumpigia kura Bwana Cruz ndio nijia ya kipekee kumzuia Trump.
Anajiunga na viongozi wengine wa Republican wanaomuunga mkono Bwana Cruz.
Image copyrightGetty
Image captionTed Cruz
Bwana Trump ameshinda majimbo mengi na kwa sasa ana takriban wajumbe 678 huku akitakiwa kujipatia wajumbe 1237 kushinda uteuzi huo.
Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment