Friday, March 18, 2016

Korea Kaskazini yarusha makombora 2 baharini



Image copyrightReuters
Image captionKorea Kaskazini yarusha makombora mawili baharini
Taifa la Korea Kaskazini limerusha makombora mawili ya masafa marefu katika bahari ya mashariki ya pwani yake,siku chache baada ya kiongozi wake Kim Jong-un kuagiza majaribio ya mabomu zaidi ya kinuklia na silaha nyengine.
Marekani imejibu kwa kutoa wito kwa Pyongyang kutozua wasiwasi katika eneo hilo ambao umekua juu tangu Korea Kaskazini kufanya jaribio la nne la mabomu yake ya kinyuklia mnamo mwezi Januari.
Korea Kusini imeelezea jaribio hilo la hivi karibuni kama tishio kubwa la usalama na udhabiti wa eneo hilo.
Image copyrightAFP
Image captionKorea Kaskazini
Shirika la habari la Korea Kusini Yonhap limesema kuwa kombora la pili huenda liliharibika hewani.
Ripoti za awali zilisema kuhusu kombora moja lililorushwa.
Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment