Monday, March 14, 2016

Klabu 5 za Ligi Kuu England Leo zitaingia kwenye Chungu cha kufanyia Droo ya kupanga Mechi za Nusu Fainali za EMIRATES FA CUP.


Droo ya Mechi za Nusu fainali-FA CUP

  • 15 Machi 2016

Timu hizo 5 zitakazoshiriki kombe hilo kongwe duniani ni Manchester United, West Ham, Everton, Watford na Crystal Palace, Wakati Everton.
Watford na Crystal Palace tayari zimetinga Nusu Fainali, Man United na West Ham inabidi zirudiane huko Upton katika Tarehe itakayopangwa baadae baada ya Jana Jumapili kwenda Sare 1-1 huko Old Trafford na Mshindi kutinga Nusu Fainali.
Kati ya hizi Timu 5 ni Man United pekee yenye rekodi ya kutwaa Mataji makubwa katika Miaka 20 iliyopita.
Mechi za Nusu Fainali zimepangwa kuchezwa Uwanja wa Wembley Jijini London hapo Jumamosi Aprili 23 na Jumapili Aprili 24.
Fainali ya FA CUP itachezwa pia Uwanjani Wembely hapo Mei 21.
Katika Droo ya Leo, Timu zimepewa Namba za Vipira ambavyo vitawekwa kwenye Chungu, 1 - Crystal Palace, 2 – Everto ,3 – Watford, 4 - West Ham United na Manchester United.
Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment