Akizungumza kwenye operesheni maalumu ya kubaini wizi wa maji, meneja wa Dawasco, Kanda ya Magomeni, Pascal Fumbuka alisema wamebaini wizi huo kufanyika mtaa wa Chama pamoja na Mkundunge iliyopo Sinza na Tandale jijini humo.
Alisema wizi huo wa maji unajulikana kwa jina la wizi wa nyoka ambapo wananchi wamejitengenezea laini za maji kinyemela, kwa kutumia mipira ya kawaida na kutoa maji kutoka umbali mrefu na kuyapitisha kwenye nyumba zao au kuunganisha kwenye ,matenki ya maji na kuuza bila kibali kutoka Dawasco.
Fumbuka alisema wamechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuondoa laini zote za maji kwa sababu za kiafya, kutoa elimu kwa wakazi hao kuwa hawaruhusiwi kujiunganishia maji, bali wanapaswa kuomba kuunganishiwa na Dawasco.
Alisema hatua nyingine yanayochukua ni kuweka kizimba (kioski) cha maji eneo hilo ili kuwezesha wakazi hao kuendelea kupata huduma ya maji kwa malipo nafuu na kwamba wao wenyewe ndio watakuwa walinzi wa miundombinu hiyo na kuhakikisha bili ya kizimba hicho inalipwa Dawasco.
Kwa upande wao wakazi wa Sinza na Tandale akiwemo Mzee Seif Shabani Mohamed amekiri kuwepo kwa wizi mkubwa wa maji kwenye mitaa hiyo na kusema unatokana na gharama kubwa za kuunganishiwa huduma hiyo pamoja na urasimu .
No comments:
Post a Comment