Monday, March 28, 2016

Aliyemzuilia msichana miaka 2 Japan akamatwa




KompyutaImage copyrightAP
Image captionPolisi wakibeba kompyuta ya Kabu Terauchi
Polisi nchini Japan wanamzuilia mwanamume wa umri wa miaka 23 anayetuhumiwa kumzuilia mateka msichana kwa miaka miwili jijini Tokyo.
Msichana huyo wa umri wa miaka 15 alifanikiwa kutoroka na kuwafahamisha polisi baada ya mwanamume huyo kutoka na kusahau kufunga mlango.
Polisi walimkamata mwanamume huyo kilomita 100 kutoka mji wa Tokyo katika jimbo la Shizuoka.
Inaaminika alijaribu kujiua.
Image copyrightAP
Mwanamume huyo anadaiwa kumteka nyara msichana huyo Machi 2014 akijifanya kuwa wakili aliyekuwa akishughulikia kesi ya talaka ya wazazi wake.
Polisi walitoa kibali cha kukamatwa kwa mwanamume huyo aliyetambuliwa kama Kabu Terauchi Jumapili.
Msichana huyo hajaonekana kudhuriwa kwa njia yoyote, vyombo vya habari nchini humo vimeripoti.
Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment