Wednesday, April 6, 2016

WATUMISHI HEWA 4,317 WAFUTWA KAZI SERIKALI KUU


KAIRUKI

AGIZO la Rais John Magufuli la kuwataka viongozi sehemu za kazi kuondoa watumishi hewa, limesaidia watumishi hewa 4,317 wa Serikali Kuu kufutwa baada ya kufanya uhakiki katika kipindi cha mwezi mmoja kuanzia Machi mosi hadi Aprili 4, mwaka huu.KAIRUKIWaziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Angela Kairuki alisema jana kuwa idadi hiyo inafanya watumishi hewa ambao wameshatambuliwa kwenye mfumo wa malipo wa serikali kuanzia Januari mwaka huu hadi juzi kufikia 7,795 na walishalipwa Sh bilioni 7.6 tangu waache kuwa watumishi wa umma.

Kairuki alisema mishahara hewa ni tatizo kubwa na linatokana na baadhi ya maofisa utumishi wa idara na taasisi za Serikali kutokuwa waaminifu.

“Hili ni eneo ambalo tunatumia asilimia 51 ya makusanyo ya TRA kwa ajili ya mishahara ni lazima tatizo hili tuliondoe,” alisema Kairuki.

Alifafanua kuhusu watumishi hao kuwa kati ya watumishi hewa 4,317, waliobainika ndani ya mwezi mmoja, watumishi 3,033 waligundulika mara tu baada ya Rais John Magufuli kutoa tamko Machi 15.

Alisema baadhi ya watumishi hao walishafariki, wengine walishastaafu na wengine ni majina bandia yaliingizwa na wajanja ili wawe wanachukua mishahara yao.

Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment