Wednesday, April 20, 2016

UMEYA WA JIJI LA TANGA GIZA NENE



tangatanga

Mgogoro wa Umeya Jiji la Tanga umetokea kufuatiwa kile kinachodaiwa kuchakachuliwa kwa matokeo ya Chama cha Wananchi CUF na kupewa ushindi kwa Chama cha Mapinduzi (CCM katika uchaguzi uliofanyika Desemba 19 mwaka jana ambapo CUF wakiwakilishwa na Rashid Jumbe ilipata kura 20 huku CCM wakiwakilishwa na Selemani Mustafa nakuambulia kura 17.

Matokeo hayo yalidaiwa kupinduliwa na Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji ambaye kwa sasa amehamishwa, na kusomeka kuwa CCM 19, CUF 18, ambapo wakala wa CUF Khalid Rashid alipinga palepale kwani alidai matokeo yalikuwa CCM 17 CUF 20 baada ya zoezi la kuhesabu kura kurudiwa.

Baada ya hayo, April 7, mwaka huu Chama cha Wananchi (CUF) kupitia Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho bara Magdalena Sakaya kumuomba Rais Magufuli na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuingilia kati mgogoro wa Umeya katika Jiji la Tanga baada ya juhudi mbalimbali za kudai haki kugonga mwamba.Magdalena Skaya

Wakati ombi hilo likisubiriwa, kwa mujibu wa Naibu Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Abdul Kambaya ameiambiamtembezi.com katika mahojiano maalumu kuwa hakuna kilichojibiwa na mpaka sasa madiwani watano (5) akiwemo aliye gombea Umeya kupitia CUF wanashikiliwa na Jeshi la Polisi, nakufanya kuendeleza sintofahamu juu ya mchakato mzima; jambo ambalo Kambaya ameshauri kuwa kama jambo hilo halitapatiwa ufumbuzi wa haraka basi Maendeleo ya Jiji la Tanga yatachelewa na kimsingi wananchi ndio watakaoumia.ABDUL CUF

Kuhusu hatua ambazo wamepanga kuchukua kama mgogoro huo hautatatuliwa Kambaya amesema kwa sasa bado wametoa muda wa kutosha ili lishughulikiwe kikamilifu na kama litashindikana basi watalikabidhi kwa wananchi muda utakapofika.

Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment