Tuesday, April 5, 2016

Wabunge watakiwa kuamua kati ya Zuma na Katiba


Image copyrightGetty Images
Image captionZuma
Kiongozi wa chama kikubwa zaidi cha upinzani nchini Afrika Kusini, amesema kuwa wabunge wa taifa hilo sasa wanafaa waamue kati ya Rais Jacob Zuma na katiba ya nchi.
Rais Zuma anafaa kujadiliwa bungeni hii leo Jumanne, na kuamua hatma yake kutokana na kashfa kubwa inayomkabili baada ya kutumia pesa za umma kujenga maskani yake ya kibinafsi ya Nkandla.
Mjadala huo utaamua kura ya kutokuwa na imani naye.
Image copyrightGetty
Image captionNyumba ya Nkandla ya Zuma
Juma lililopita mahakama ya juu zaidi nchini humo iliamua kuwa bwana Zuma alikiuka katiba kwa kutumia mamilioni ya dola kujengea maskani hayo ya kibinafsi.
Unknown Web Developer

Morbi aliquam fringilla nisl. Pellentesque eleifend condimentum tellus, vel vulputate tortor malesuada sit amet. Aliquam vel vestibulum metus. Aenean ut mi aucto.

No comments:

Post a Comment