Rais wa Sudan Omar al-Bashir ameanza ziara ya siku tano katika jimbo la Darfur kutafuta uungwaji mkono wa azimio lake la kuinganisha jimbo hilo na Sudan
Ziara hiyo inalenga kupigia debe hoja ya muungano wa jimbo hilo lililosakamwa na vita na kusababisha vifo vya watu 300,000 tangu mapigano baina ya waasi na majeshi ya serikali.
Yamkini Al Bashir ambaye anatafutwa na mahakama ya uhalifu wa kivita yenye makao yake makuu nchini Uholanzi amekwenda Darfur ilikunadi sera ya muungano huku jimbo hilo likitarajiwa kupiga kura ya maoni kuhusu iwapo litajitenga au lijiunge na Sudan katika mpango wa jimbo la tano.
Bashir anakanusha madai dhidi yake.
Katika mji mkuu wa jimbo la Darfur, El-Fasher, Bashir alilakiwa kwa nyimbo za kitamaduni na densi na maelfu ya wafuasi wake.
Kama kawaida yake Bashir angependa kuungana kwa jimbo hilo.
No comments:
Post a Comment