"Watu Sahara magharibi watalazimika mara nyingine tena kutetea haki zao kwa njia zote halali, ikiwa ni pamoja na mapambano ya silaha, ambayo yalipitishwa na Umoja wa Mataifa kwa watu wote walio chini ya ukoloni," inasema barua kutoka kwa Bw Abdelaziz iliyotumwa kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa katika Ukanda huo (MINURSO) ulitumwa mwaka 1991 ili kufuatilia mkataba wa usitishwaji mapigano katika Sahara Magharibi kwa kusubiri kukamilika kwa sheria maalum ya eneo hilo, koloni ya zamani ya Uhispania iliyounganishwa na Morocco mwaka 1975.
Wakati wa ziara yake katika Ukanda huo mapema mwezi Machi, Ban Ki-moon alikemea vikali mwenendo wa Rabat inayolichukulia eneo la Sahara Magharibi kama sehemu yake.
Kwa kujilipiza kisasi, Morocco iliwafukuza baadhi ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa na kufunga ofisi ndogo ya kijeshi ya Umoja huo. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, hatua hizo zinauzuia kufanya kazi.
No comments:
Post a Comment